IQNA

Qur'ani Tukufu Inasemaje / 38

Ni jambo gani huifanya sadaka ikose thamani na ibatilike

17:45 - November 27, 2022
Habari ID: 3476155
TEHRAN (IQNA) – Waumini wanapaswa kuchukua tahadhari wasifanye sadaka zao kuwa batili na zikose thamani kwa maudhi na matamshi yasiyofaa.

Qur'ani Tukufu ina mifano miwili kuhusu motisha au nia zisizo sahihi katika kutoa sadaka ambapo inaonyesha jinsi tabia kama hiyo ilivyo mbaya na isiyo na maana.

Mojawapo ya mienendo mikuu ya kimaadili katika jamii inayochochewa na waja wema kuwasaidia wenye uhitaji kwa njia mbalimbali. Hata hivyo, kama misaada hii haitatolewa kwa njia sahihi, sio tu kwamba haitakuwa na athari chanya za kijamii bali malipo ya amali njema huko akhera pia yanaweza kubatilishwa.

Qur'ani Tukufu ina ushauri mwingi kuhusu hili, ukiwemo ule ulio katika aya ya 264 ya Surah Al-Baqarah:

 Enyi mlio amini! Msiharibu sadaka zenu kwa masimbulizi na maudhi, kama anaye toa mali yake kwa kuwaonyesha watu, wala hamuamini Mwenyezi Mungu wala Siku ya Mwisho. Basi mfano wake ni kama mfano wa jabali ambalo juu yake pana udongo, kisha likapigwa na mvua kubwa, ikaliacha tupu. Basi hawatakuwa na uweza wowote kwa walivyo chuma. Na Mwenyezi Mungu hawaongoi watu makafiri.”

Tafsiri ya Nemouneh wa Qur'ani Tukufu inasisitiza kwamba katika aya hii, Qur'ani Tukufu inatumia mifano miwili kuonyesha jinsi tabia mbaya inavyofanya kutoa sadaka kutokuwa na thamani na ubatili.

Mfano wa kwanza ni: “(Mtu huyo) ni kama anayetoa mali yake kwa ajili ya kujionyesha kwa watu na hamwamini Mwenyezi Mungu wala Siku ya Mwisho.”

Mfano unaofuata ambao Quran inaitaja ni huu: “Basi mfano wake ni kama mfano wa jabali ambalo juu yake pana udongo, kisha likapigwa na mvua kubwa, ikaliacha tupu. Basi hawatakuwa na uweza wowote kwa walivyo chuma. Na Mwenyezi Mungu hawaongoi watu makafiri.”

Hivyo vitendo hivyo vinavyohusisha unafiki, lawama na maudhi hutoka katika mioyo migumu na watu wa aina hiyo hawanufaiki navyo.

Ujumbe wa aya kwa mtazamo wa Tafsiri ya Noor ya Qur'ani Tukufu:

  • Kuwakashifu na kuwaudhi wenye haja kunaifanya sadaka kukosa thamani. (Msifanye sadaka zenu kuwa hazina matunda...)
  • Unafiki ni dalili ya kukosa imani ya kweli kwa Mwenyezi Mungu na Siku ya Kiyama. (...Mwenye kutumia mali yake kwa kujionyesha na ambaye hana imani na Allah SWT wala kuamini Siku ya Kiyama)
  • Si jambo la kutoa sadaka bali ni makusudio ya mwenye kutoa sadaka. (… kujionyesha kwa watu)
  • Matendo ya wenye kuwatukana kuwavunjia heshima wengine hubatilisha sadaka.
  • Makusudio ya mnafiki na mwenye kujionesha hatimaye yatadhihirika.
  • Mnafiki si tu kwamba hatakuwa na malipo huko akhera bali anashindwa kukua kiroho. (Watu kama hao hawawezi kunufaika na waliyoyachuma.)
  • Wanaafiki na wanaowaumiza kihisia wenye kupokea sadaka wako katika kundi la ukafiri na wala hawataongoka. (Mwenyezi Mungu hawaongoi makafiri.)
Habari zinazohusiana
captcha