TEHRAN (IQNA) – Baada ya maandalizi kama vile kusafisha, kuosha na kupamba kwa maua, kaburi tukufu la Imam Ali (AS) huko Najaf, Iraq, limekuwa uwanja wa sherehe siku ya Ijumaa na leo, ambayo ni siku ya 13 ya mwezi wa Rajab katika Hijria Qamari na inaashiria kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Imam wa kwanza wa Waislamu wa Madhehebu ya Shia (AS).