Mwaka wa kalenda ya Kiislamu wa 1444 Hijria ulianza mwishoni mwa Julai 2022.
Kati ya Mahujaji hao, 4,329,349 walifika nchini humo kwa ndege, 507,430 walifika kupitia bandari za nchi kavu, na 3,985 walifika kupitia bandari za bahari, wizara Hija na Umrah ilisema.
Jumla ya Mahujaji 1,351,731 walifika Madina kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Prince Mohammed Bin Abdulaziz wa mji huo mtakatifu na kutembelea Msikiti wa Mtume SAW kwa ajili ya Ziyara.
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Prince Abdul Mohsin bin Abdulaziz huko Yanbu pia ulikaribisha Mahujaji 11,132 wa Umrah, wizara hiyo ilisema.
3482501