IQNA

Waislamu Marekani

Kituo cha Jumuiya ya Waislamu cha Edison, Marekani chatafuta Idhini ya Mradi wa Msikiti

15:09 - February 13, 2024
Habari ID: 3478343
IQNA - Kituo cha Jumuiya ya Waislamu cha Edison, jimboni New Jersey nchini Marekani kinataka kujenga msikiti kwenye eneo lake la Plainfield Avenue, ambalo tayari lina makao na mnara.

Shirika lisilo la faida limetuma maombi kwa Bodi ya Marekebisho ya Kugawa maeneo ya kitongoji ili kupata kibali cha kupanua na kukarabati jengo lililopo kuwa nyumba ya ibada ya ghorofa tatu yenye muundo  Afrika Kaskazini na Andalusia, kuba na mnara wa urefu wa futi 45.

Mradi huo pia ni pamoja na kutengeneza sehemu ya maegesho ya nafasi 40 za magari.

Bodi ya Ukanda itafanya kikao cha hadhara kuhusu ombi hilo mnamo Februari 20.

Kwa kuongezea, jengo lililopo lingekarabatiwa kuwa vyumba vya madarasa, eneo la kutawadha na vyumba vya mikutano, nyaraka zinaonyesha.

3487171

Kishikizo: marekani msikiti
captcha